Psalms 121

Bwana Mlinzi Wetu

(Wimbo Wa Kwenda Juu)


1 Nayainua macho yangu nitazame vilima,
msaada wangu utatoka wapi?

2 aMsaada wangu hutoka kwa Bwana,
Muumba wa mbingu na dunia.


3 bHatauacha mguu wako uteleze,
yeye akulindaye hatasinzia,

4 chakika, yeye alindaye Israeli
hatasinzia wala hatalala usingizi.

5 d Bwana anakulinda,
Bwana ni uvuli wako mkono wako wa kuume,

6 ejua halitakudhuru mchana,
wala mwezi wakati wa usiku.

7 f Bwana atakukinga na madhara yote,
atayalinda maisha yako,

8 g Bwana atakulinda unapoingia na unapotoka,
tangu sasa na hata milele.
Copyright information for SwhKC